Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2017

Coming Soon: Daraja Juu ya Mto Nile (English Edition)

The book titled: DARAJA JUU YA MTO NILE authored by Mark Mwandosya, was published in 2015. The publication of the book in kiswahili was aimed at, among other reasons, the promotion of the use of kiswahili, a national language of Tanzania, and Kenya, and a language widely spoken in Eastern Africa and beginning to spread across Africa and other continents. Yet english, as a language is more widely spoken and indeed the "kiswahili of the world". Calls have been made for the book to be translated into english, and the author has obliged. For the subject of transboundary watercourses is as topical as it is current. The River Nile is no exception. The book: BRIDGE ACROSS THE RIVER NILE is with the printers and should be out in a few weeks. ©Mark Mwandosya

Salaam kutoka Comoro

Nimeona niandike waraka huu kutoka ughaibuni, ingawa si ugenini sana, nikiwa Jamhuri ya Comoro. Nimebahatika kusafiri sana kikazi duniani kote, kuanzia Japan mpaka Brazil, kuanzia Guyana mpaka Australia. Nimeiwakilisha nchi kikazi katika mabara yote isipokuwa Aktiki na Antaktika. Namshukuru Rabuka kwa kuniwezesha kulitumikia Taifa langu kwa zaidi ya miaka arobaini. Nimetembelea nchi zote jirani isipokuwa Jamhuri ya Comoro. Mara nyingi tumezoea kusema Tanzania inapakana na nchi nane; Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Watu ya Congo, Zambia, Malawi, na Msumbiji. Tunasahau kwamba watu wa Visiwa vya Comoro ni jirani zetu. Badala ya mpaka wa ardhi tunatenganishwa na Bahari ya Hindi. Inawezekana hii ikawa ndio sababu ya nchi zetu kutokuwa na ushirikiano wa karibu kiuchumi na kiutawala, pamoja na kwamba kijamii na kiutamaduni sisi, na hasa watu wa mwambao wa pwani na Zanzibar, Wacomoro wamekuwa ni sehemu yetu. Mara nyingi utasikia fulani na fulani wametutangulia mbele